Showing posts with label habari za nje. Show all posts
Showing posts with label habari za nje. Show all posts

Thursday, 11 July 2013

KENYA YAONGOZA KWA UFISADI


Kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Transparency International, Kenya imeshika nafasi ya nne kwa ufisadi ikiwa ni  miongoni mwa nchi 107 ambako utafiti huo ulifanywa.
Ripoti hiyo ilibaini kwamba Wakenya saba kati ya 10 waliohojiwa walisema wamewahi kutoa hongo maishani mwao ili waweze kupata huduma moja hadi nane kati ya zilizochunguzwa.
Kulingana na utafiti huo, maofisa wa polisi ndio waliopatikana kuwa mafisadi zaidi nchini wakifuatiwa na wabunge, vyama vya kisiasa, mahakama na wafanyakazi wa Serikali.
Wakenya wengi walisema vyombo vya habari, mashirika yasiyo ya kiserikali na taasisi za kidini hazina ufisadi mwingi.
Nchi fisadi zaidi duniani ni Sierra Leone ambako asilimia 84 ya watu waliohojiwa walikubali kwamba wametoa hongo. Sierra Leone inafuatwa na Liberia (asilimia 75) na Yemen (asilimia 74).
Nchi ambazo zilipatikana kuwa na ufisadi finyu ni Finland, Japan, Australia, Denmark, Uhispania, Canada, Ureno, Uruguay, Norway, New Zealand, Korea Kusini na Malaysia ambako watu zaidi ya 95 kati ya 100 waliohojiwa walisema hawajaona ufisadi wowote nchini mwao.
Katika eneo la Afrika Mashariki, Kenya ndiyo nchi fisadi zaidi ikifuatwa na Uganda (asilimia 61) na Tanzania (asilimia 56). Kulingana na utafiti huo ambao watu 114,000 walihojiwa, Rwanda ilipatikana kuwa na ufisadi mdogo zaidi katika eneo la Afrika Mashariki. Raia 13 pekee kati ya 100 wa nchi hiyo walikubali mwamba wametoa hongo. Ufisadi ulipatikana kukithiri zaidi barani Afrika. Baadhi ya nchi fisadi zaidi Afrika ni Zimbabwe, Msumbiji, Libya na Cameroon (zote zikiwa na asilimia 62) na Nigeria (asilimia 44).

Wednesday, 10 July 2013

OBAMA KAIANZIA KAZI TANZANIA:AMCHAGUA AMSAIDIZI WAKE WA KARIBU KUWA BALOZI WA TANZANIA


Rais wa Marekani Barrack Obama amemteua msaidizi wake wa karibu, Mark Childress kuwa balozi wa nchi hiyo, hapa nchini.
Childress ni msaidizi wa Obama katika Ikulu ya Marekani (White House) akiwa Naibu Mkuu wa Utumishi anayeshughulikia mipango katika Serikali ya nchi hiyo na aliwahi kufanya kazi katika Bunge la Seneti.
Obama amefanya uteuzi huo ikiwa ni wiki moja tangu alipohitimisha ziara yake katika nchi tatu za Bara la Afrika, Tanzania ikiwa mojawapo. Pia alizitembelea Senegal na Afrika Kusini.
Hata hivyo, taarifa iliyotolewa na Ikulu ya Marekani jana ilisema nafasi hiyo inahitaji kuidhinishwa na Bunge la Seneti la nchi hiyo. Uteuzi wake unaweza kuwa na maana kubwa katika kutekeleza sera za nje za Marekani.
Katika miaka ya karibuni, Tanzania imeshuhudia ziara za viongozi wakuu wa nchi hiyo nchini ambao ni Bill Clinton, George Bush na Obama.
Kuteuliwa kwa Childress, kunaashiria kwamba Balozi wa sasa wa Marekani nchini Alfonso Lenhardt anakaribia kumaliza muda wake.
Awali, Childress ambaye aliwahi kuwa msaidizi na msiri wa muda mrefu wa Seneta wa zamani, Tom Daschle, alitarajiwa kushika moja ya nyadhifa mbili katika utawala wa Rais Obama ambazo ni Mkuu wa Utumishi katika Idara ya Huduma ya Afya ya Jamii (HHS) au Naibu Mkurugenzi katika Ofisi ya Maboresho ya Afya katika Ikulu ya Marekani.
Hata hivyo, jina lake liliondolewa katika mapendekezo ya uteuzi wa kuongoza ofisi hizo baada ya kuhusishwa katika masuala ya kodi Februari 2009, hivyo kubaki pasipo na jukumu maalumu.
Pamoja na mkanganyiko uliojitokeza awali kuhusu majukumu yake, Childress alimudu kufanya kazi kubwa katika kuwezesha kupitishwa kisha kutekelezwa kwa mabadiliko makubwa katika sekta ya afya ya nchi hiyo. Aliteuliwa kuwa Naibu Mkuu wa Utumishi wa Marekani, 2012.
Mwaka 2009, mpigania mabadiliko na maboresho ya sekta ya afya Marekani ambaye sasa ni Seneta, Edward M. Kennedy alimwomba Childress kujiunga na timu yake ya ushauri wa masuala ya afya, elimu, wafanyakazi na pensheni.
Timu hiyo pia ilikuwa na kazi ya kumshauri kuhusu masuala ya mabadiliko ya afya na Childress alikuwa miongoni mwa watu walioshiriki kutoa rasimu ya kwanza ya muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Afya 2009.
Baada ya muswada huo kupitishwa Februari 2010, Childress aliondoka katika kamati hiyo na kujiunga na Idara ya Huduma ya Afya ya Jamii Marekani ambako alikuwa na wajibu wa kusimamia utekelezaji wa sheria hiyo mpya akiwa Kaimu Msimamizi Mkuu wa idara hiyo.

MAISHA YA OSAMA KABLA HAJAKAMATWA YAFICHULIWA


TUME ya Abbottabad imesema kuwa Osama bin Laden aliishi kama mtu wa kawaida bila wasiwasi wowote kwa karibu miaka 10 na aliwahi hata kusimamishwa na polisi katika eneo la Swat huko Pakistan kwa kupeleka gari kwa kasi mno, lakini hakukamatwa.
Ripoti hiyo iliyofichuliwa na Televisheni ya al Jazeera na kuoneshwa juzi jioni, inaonesha kinagaubaga maelezo ya kusisimua kuhusu maisha ya Osama bin Laden, mtu hatari aliyekuwa akitafutwa kwa udi na uvumba, na aliyekuwa akivaa kofia la mchunga ng’ombe katika tambarare za Marekani, kuepuka kugunduliwa kutoka angani.
Ripoti hiyo ya kurasa 336, iliandikwa na tume ya Abbottabad inayoongozwa na jaji na iliyoundwa na Serikali ya Pakistan muda mfupi baada ya vikosi maalumu vya Marekani kumuua bin Laden Mei 2 mwaka 2011. Misingi ya ripoti hiyo ni mahojiano yaliyofanywa na vyanzo 201, wakiwemo jamaa wa familia yake na maofisa mbalimbali.
Matokeo ya uchunguzi huo ambayo hayajachapishwa rasmi, yanajumuisha ushahidi wa uzembe mkubwa katika karibu kila ngazi ya vyombo vya usalama vya Pakistan.
Ripoti inakosoa vikali namna Marekani ilivyofanya uvamizi katika makazi ya bin Laden huko Abbottabad, ikisema ilichukua hatua kama jambazi mhalifu. Inauweka katika kiti moto utawala wa Pakistan kwa kushindwa kugundua shughuli za Shirika la Ujasusi la Marekani (CIA), katika ardhi yake, na hautupilii mbali uwezekano wa kuhusika maofisa walaghai katika idara ya ujasusi ya Pakistan, suala tete kuligusia katika uchunguzi wa hali ya juu namna hiyo.
Ripoti inatoa maelezo kuhusu usiku wa kifo cha bin Laden na kutoa taswira ya mtu aliyekuwa akibabakia na kama mwenda wazimu ambaye kila mara alikuwa mbioni kukwepa kutiwa mbaroni.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo, Bin Laden aliwasili nchini Pakistan msimu wa machipuko mnamo mwaka 2002, na wakati mmoja aliishi Haripur kwa miaka miwili kabla kuhamia katika makazi yake ya mjini Abbottabad na familia yake kubwa mnamo Agosti 2005.
Ripoti inasema maeneo yote alikoishi hayajulikani kikamilifu, lakini miongoni mwao ni FATA yani Waziristan kusini na Bajaur, Peshwar, Swat na Haripur.
Ripoti imegundua bin Laden aliingia Pakistan akitoa eneo la Tora Bora nchini Afghanistan, ambako majeshi ya Marekani yalikuwa yakimsaka mwaka 2002. Familia yake ilihamia Karachi, Pakistan kutoka Kandahar, muda mfupi baada ya mashambulio ya Septemba 11, 2001 nchini Marekani dhidi ya jengo la Shirika la Biashara la Kimataifa (WTO) mjini New York, makao makuu ya wizara ya ulinzi, Pentagon nje ya mji wa Washington, na uwanja mmoja huko Pennsylvania.
Osama hakupenda mali
Katika ushuhuda wao wake wa bin Laden walisema hakupenda sana mali zake binafsi na alikuwa na nguo chache sana. Ripoti hiyo imesema kabla kwenda Abbottabad bin Laden alikuwa na mavazi matatu ya kitamaduni yajulikanayo kama shalwar kameez aliyoyavaa wakati wa msimu wa kiangazi na mengine matatu kwa ajili ya msimu wa baridi.
Wakati alipojihisi anaugua, Osama bin Laden alijitibu mwenyewe kutumia dawa za kienyeji za Kiarabu. Kwa mujibu wa ripoti zisizo rasmi za Marekani, bin Laden alikuwa akiugua ugonjwa wa Addison, upungufu wa adrenalini mwilini, na kila mara alipojihisi mvivu angekula tufaha na chokoleti.
Maofisa wa Serikali na usalama nchini Pakistan hawakuweza kupatikana ili kutoa kauli kuhusu ripoti hiyo. Baadhi ya maofisa wa Marekani wameelezea wasiwasi wao wakiyashuku mashirika ya ujasusi ya Pakistan kwa kumlinda bin Laden, lakini Pakistan imelipuuzilia mbali wazo hilo.

MANDELA APUMULIA MASHINE..MADAKTARI WAPANGA KUIZIMA


MADAKTARI wanaomtibu Rais Mstaafu wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, wanakubali kuwa kiongozi huyo basi tena kwani hali yake ni tata na sasa wanasubiri kiungo kimojawapo cha mwili wake kishindwe kufanya kazi ndipo wazime mashine inayomsaidia kupumua.

Kutokana na subira hiyo madaktari hao sasa wamebadili msimamo wao wa awali wa kuiondoa mashine hiyo inayomsaidia kupumua.
“Madaktari hao, wameishauri familia yake kuachana na ushauri wa awali wa kuiondoa mashine hiyo hadi tu pale moja ya kiungo chake muhimu cha mwili kitakaposhindwa kufanya kazi,” alisema rafiki wa Mandela, Denis Goldberg ambaye alikuwa mpigania uhuru aliyewahi kufungwa pamoja na Mandela.
Amesema madaktari hao waligusia kuhusu suala la kuondoa mashine lakini baadaye walikataa kwa kuwa kiongozi huyo aliweza kusogeza baadhi ya viungo na kutambua sauti.
“Ni kweli kuwa hali ya Mandela ni mbaya lakini si kama ambavyo baadhi ya vyombo vya habari vimekuwa vikiandika,” alisema Goldberg.
Juzi vyombo vya habari vya hapa nchini vilitoa hati ya kiapo ya mahakama, ikionyesha kuwa madaktari hao waliishauri familia ya Mandela kuondoa mashine ya kumsaidia kupumua kwani asingeweza kuendelea kuishi.
Hata hivyo, msemaji wa Rais Jacob Zuma,Mac Maharaj alikataa kuzungumzia kuhusu hati ya mahakama ambayo ilieleza kuwa Mandela mwenye miaka 94 yupo mahututi.

In Kampala: Museveni in S. Sudan for Independence anniversary



Museveni in S. Sudan for Independence anniversary
 
 President Yoweri Museveni
newvision
By Francis Apiliga

Hundreds of thousands of South Sudanese and the foreign nationals Tuesday gathered at Dr. John Garang Mausoleum to celebrate the second year of independence under the theme: ‘Towards effective nation building and prosperity for all’.

 “We celebrate the birth and death our heroes and martyrs. We must not forget that we have been born of the blood and sacrifice of our founding members like the Dr. John Garang,” President Salva Kiir said while addressing the mammoth crowd in Juba City.

The president said those who doubted the survival of South Sudan after its separation from the Khartoum have been proved wrong by the resilience and solidarity of the South Sudanese.

He listed the passing of at least 19 legislations such as the Education Act, The Agriculture Act and the Media bills which he said have also been passed by the parliament awaiting his amendment as key achievements in the democratization process.

The completion of Juba-Nimule road, the establishment of the National Electoral Commission and the National Constitutional Review Commission are key other achievements in the Second Year of Independence.

Kiir also announced that the oil refinery in Bentiu would be opened in August this year. “We have also increased our non-oil revenue from 7 million to 100 million South Sudanese pounds (SSP) which is an increase of more than 800%,” he said.

He promised to increase the salaries of teachers, soldiers and continue to empower youth and women as well as creating jobs for the youth through encouraging infrastructure development and private sector promotion.

On corruption, the president said: “Corruption will not be tolerated. Any body found guilty will be taken to the court of law. The time for impunity is no more. No one is above the law,” he said.

“I am also troubled by the increasing crime rate in our cities. Much as we may blame external factors for the increased crime, the police should have done better. Some of them are very indiscipline. This is a very serious crime, lets come back to our senses,” the Kiir said.

The president also said his government is committed to the Cooperation Agreement with Sudan. According to Kiir, the Abyei people of deserve a final resolution.

He condemned the acts of David Yau Yau in Pibor, Jonglei State but also warned the national army officials accused of committing abuses that they will not go scout-free.

At least four foreign heads of state including Presidents Museveni of Uganda, Paul Kagame of Rwanda, Ian Khama of Botswana, Hassan Mohamud of Somalia and the former South African president Thabo Mbeki and several foreign dignitaries attended the occasion marked yet again with pomp, glamour and enthusiasm.

Tuesday, 9 July 2013

In Kampala: Deputy Speaker orders inquiry into drivers’ strike


 
Deputy Speaker orders inquiry into drivers’ strike 
Striking drivers in Jinja stopping a taxi that was carrying passengers. PHOTO/Donald Kiirya
newvision
By Moses Walubiri & Mary Karugaba

KAMPALA - The Physical Infrastructure Committee of parliament is set to interface with striking taxi drivers and other stakeholders as attempts to end a strike that has paralyzed public transport gathers pace.

This followed an order on Tuesday by Deputy Speaker of Parliament Jacob Oulanyah for the committee to table a report on the strike to the House over a host of grievances that have seen a sit down strike by taxi operators in Mityana, Bugiri, Kasese, Jinja, Iganga and Mbale enter its second week.

“Let the committee on Physical Infrastructure meet drivers and the other stakeholders over this issue,” Oulanyah said after Mukono Municipality MP, Betty Nambooze, raised the drivers’ grievances.

She told the House that one of the reasons the drivers have gone on strike is the “exorbitant fees” in taxes they pay to different local government entities on the routes they ply.

The legislator said that if, for example, a taxi plied the route between Mbale to Kampala, its operator would have to pay money to Kampala Capital City Authority, and city councils of Jinja, Iganga, Bugiri and Mbale.

These fees, she averred are over sh900, 000, accusing government of imposing stringent express traffic fines in an ad hoc manner.

Transport Minister Abraham Byandala, however, ruled out going back on government’s decision to impose stringent express traffic fines saying: “I cannot sit down and see Ugandans die in senseless road accidents. We shall make sure that sanity prevails on our roads.”

Byandala rejected Nambooze’s submission that hiked traffic fines will cause a spike in transport fares, describing the fines as “voluntary.”

“It’s those who commit traffic offenses who will continue paying these fines. It’s not a kind of tax that will be imposed across the board,” Byandala said.

The development comes at a time when transport fares to Eastern Uganda have short up over the ongoing strike.

Last week, drivers in Busoga packed their car and blocked the Jinja-Kampala highway in protest over the revised traffic scheme.

MANDELA APUMULIA MASHINE..MADAKTARI WAPANGA KUIZIMA


MADAKTARI wanaomtibu Rais Mstaafu wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, wanakubali kuwa kiongozi huyo basi tena kwani hali yake ni tata na sasa wanasubiri kiungo kimojawapo cha mwili wake kishindwe kufanya kazi ndipo wazime mashine inayomsaidia kupumua.

Kutokana na subira hiyo madaktari hao sasa wamebadili msimamo wao wa awali wa kuiondoa mashine hiyo inayomsaidia kupumua.
“Madaktari hao, wameishauri familia yake kuachana na ushauri wa awali wa kuiondoa mashine hiyo hadi tu pale moja ya kiungo chake muhimu cha mwili kitakaposhindwa kufanya kazi,” alisema rafiki wa Mandela, Denis Goldberg ambaye alikuwa mpigania uhuru aliyewahi kufungwa pamoja na Mandela.
Amesema madaktari hao waligusia kuhusu suala la kuondoa mashine lakini baadaye walikataa kwa kuwa kiongozi huyo aliweza kusogeza baadhi ya viungo na kutambua sauti.
“Ni kweli kuwa hali ya Mandela ni mbaya lakini si kama ambavyo baadhi ya vyombo vya habari vimekuwa vikiandika,” alisema Goldberg.
Juzi vyombo vya habari vya hapa nchini vilitoa hati ya kiapo ya mahakama, ikionyesha kuwa madaktari hao waliishauri familia ya Mandela kuondoa mashine ya kumsaidia kupumua kwani asingeweza kuendelea kuishi.
Hata hivyo, msemaji wa Rais Jacob Zuma,Mac Maharaj alikataa kuzungumzia kuhusu hati ya mahakama ambayo ilieleza kuwa Mandela mwenye miaka 94 yupo mahututi.

"NASUBIRI WAKATI MWAFAKA WA KUMUONYESHA KIKWETE YA KWAMBA MIMI NI NANI".....HILI NI TISHIO LA KIHUNI LA RAISI KAGAME WA RAIS KIKWETE


Nikiwa  katika  upekuzi  wangu, nimeshtushwa sana na kauli za  KIHUNI  za Rais  Paul Kagame  dhidi ya  Rais wetu Kikwete na nchi yetu kwa ujumla....

Rais Kikwete ameepuka malumbano na Kagame kwa  kukaa  kimya , lakini inaelekea Kagame  anadhani ukimya wa Kikwete ni uoga kwake  au labda anatafsiri kuwa anadharauliwa.....

Nadhani  huu  ni  wakati  mwafaka  kwetu  sisi  watanzania  kuungana  na  kumuunga  mkono  rais  wetu  juu  ya  huu  UPUMBAVU  wa  Kagame....

Kagame  ni  lazima  atambue  kwamba  watanzania  tupo  tayari  kuilinda  nchi  yetu  kwa  gharama  yoyote  na  kamwe  hatuwezi  kuwa  VIBARKA  wa  Rwanda...

Ifuatayo  ni  Kauli  ya  Kihuni  aliyoitoa  Rais  Kagame  Kwa  Taifa  letu:
-------------------------------------------------------------

.....“Those people [Tanzanian President Jakaya Kikwete] you just heard siding with Interahamwe and FDLR and urging negotiations… negotiations? 


 Me, I do not even discuss this topic, because I will just wait for you [Tanzanian President Jakaya Kikwete] at the right place and I will hit you! He[Tanzanian President Jakaya Kikwete] did not deserve my answer.


 I did not waste my time answering him…It is well known. There is a line you cannot cross, there is a line, a line that you should never cross. It is impossible…”“


It is in these ominous terms that the Rwandan dictator General Paul Kagame threatened to get even with Tanzanian President Jakaya Kikwete, while addressing Rwandan Youth on June 30, 2013 during a summit called “Youth Konnect”“, sponsored by his wife, Janet Kagame.


Relations between Tanzanian President Jakaya Kikwete and Rwandan leaders have soured in the last weeks. On several occasions Rwandan leaders called the Tanzanian President “a genocide and terrorist sympathizer”, “ignorant”, “arrogant”, and “mediocre leader”. 

The relations have deteriorated following the recommendation by President Jakaya Kikwete of open negotiations between Rwandan, Ugandan and Congolese leaders and their respective armed opposition in order to bring durable peace and security in the African Great Lakes region....
 


source..I will Just Wait For You At the Right Place And I will Hit You, Rwandan General Paul Kagame Threatens Tanzanian Jakaya Kikwete

NANDO NA FEZA KESSY WAENDELEA KUPEPERUSHA BENDERA YA TANZANIA NDANI YA BIG BROTHER......HAKUNA ALIYEINGIA KIKAANGONI


 
Wiki hii Watanzania na mashabiki wa shindano la Big Brother Africa hawana haja ya kuwa wasiwasi ya kuwaokoa washiriki wao kwakuwa Nando na Feza Kessy wako safe. 


Kilichobaki ni kuvuta tu viti virefu na kuendelea na bata huku tukiwaangalia wengine wakihaha kuokoa washiriki wao.


Hata hivyo Evictions ya wiki hii inatarajiwa kuwa ya aina yake tangu show ianze hasa kwakuwa waliotajwa kuondoka ni washiriki ngangari.

 Ni nani kati ya Cleo, Natasha, Pokello, Selly, Melvin na Annabel anayeweza kubwaga manyanga kwenye mchezo huo wa ‘kufukuzana’? Afrika itaamua.

WATOTO WAWILI WALIOKUWA WAMEPELEKWA "JANDONI" WAMEFARIKI WA AJALI YA MOTO HUKO LINDI


 Lindi- Watoto wawili wamekufa na mmoja wao kunusurika mauti, baada ya kuungua kwa moto uliosababishwa na kibatari kilichounguza nyasi za kijumba walichokuwemo.

Kaimu Kamanda wa Mkoa wa Lindi, Renata Mzinga amesema ajali hiyo ilitokea mwishoni mwa wiki jana katika


mtaa wa Mitwero, katika kata ya Rasbura ya Manispaa ya Lindi na kuwataja waliokufa kuwa ni Maliki Kasimu (7) na na Selemani Fadhili (5) wakati aliyenusurika ni Juma Abdallah.

Mzinga amesema watoto hao watatu waliofika kwa mzee mmoja wa jadi, walikuwa wakijenga nyumba kwenye michezo yao wakati wakiwasubiri wenzao wafike siku za usoni, tayari kwa shughuli ya jando.

Siku ya tukio, moto huo ulishika nyasi zilizokuwa ndani ya shimo na kuwaka na kuwachoma Maliki na Selemani ambapo mwenzao, Juma alifanikiwa kukimbia na kujiokoa.

Wanakijiji wanasema mwangalizi wa jando hilo alikuwa mbali na eneo la tukio na hivyo kushindwa kuwaokoa