Mr Nice ambaye bado yuko Kenya anatarajia kujiunga na label nyingine nchini humo ‘Candy Records’ ambayo ina miezi michache toka ianzishwe.
Kwa mujibu wa CEO wa label hiyo John Kariuki aliyekuwa akizungumza katika ufunguzi rasmi wa label hiyo jijini Nairobi, alisema wako katika hatua za mwisho kukamilisha mpango wa Mr Nice kusain mkataba nao kama ilivyoripotiwa na Niaje.
Label hiyo tayari imesha wasain wasanii kadhaa wa Afrika Mashariki akiwemo hit maker wa ‘Ulofa’ Top C wa Tanzania, pamoja na wengine kutoka Kenya.
0 comments:
Post a Comment