Ramadhan Seleman ‘Rama Mla watu’, aliyekuwa akishikiliwa na
dola kwa tuhuma za mauaji ya mtoto, Salome Yohana licha ya kuondolewa
hatia hiyo huku akiwekwa chini ya uangalizi baada ya kubainika kuwa na
matatizo ya akili, Jumatano iliyopita alirudishwa hospitali ya waalifu
ya Isanga iliyopo Mirembe, Mkoani Dodoma.
Rama alipandishwa basi ya Shukrani majira ya saa moja asubuhi akiwa na
askari wawili waliokuwa wakimlinda kuhakikisha wanamfikisha kwenye
hospitali hiyo, mpaka akili yake itakapotengemaa ndipo ataachiwa
uraiani.
Kijana huyo alisafirishwa kupelekwa hospitalini huko kufuatia amri iliyotolewa na Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam katika kesi yake ya mauaji iliyokuwa ikiwakabili na mama yake, Khadija Musa, baada ya kubainika kuwa alitenda kosa hilo akiwa na matatizo ya akili.
Kijana huyo alisafirishwa kupelekwa hospitalini huko kufuatia amri iliyotolewa na Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam katika kesi yake ya mauaji iliyokuwa ikiwakabili na mama yake, Khadija Musa, baada ya kubainika kuwa alitenda kosa hilo akiwa na matatizo ya akili.
0 comments:
Post a Comment