Mtuhumiwa namba mbili Joseph
Ludovick (kulia) wa kesi ya kula njama za kutaka kumteka na kumdhuru
Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Mwananchi, Denis Msacky, akitoka nje ya
Mahakama ya Hakimu Mkazi Dar es Salaam jana baada ya kuachiwa kwa
dhamana. Kushoto ni rafiki yake, Hamfrey Masawe. (Picha na Venance
Nestory)
NA FLORA MWAKASALA
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini
Dar es Salaam, imemwonya mshitakiwa mwenza wa Mkurugenzi wa Ulinzi wa
Usalama wa Chadema, Wilfred Lwakatare, Ludovick Joseph, kutozungumza na
vyombo vya habari wala mitandao ya kijamii. Hakimu Mkazi Aloyce
Katemana, alitoa onyo hilo jana baada ya Wakili Nyaronyo Kicheere,
kulalamikia kitendo cha mshitakiwa Joseph kuzungumza na waandishi wa
habari na kuchapisha habari za kesi hiyo magazetini.
0 comments:
Post a Comment